SIKU YA 18 – SIKU 21 ZA KUFUNGA NA KUOMBA

Maombi ya siku 21, Wiki ya Tatu

Siku ya 18, Tarehe 26 January 2023.

Ombi Kuu: VIONGOZI WA SERIKALI NA VYAMA.

1. Ombea mihimili mikuu mitatu; Bunge (Kutunga Sheria), Mahakama (Kutafsiri Sheria) na Serikali (Kutekeleza Sheria) Zaburi 22:28, 1Timotheo 2:1-4.

♦ Ombea kila muhimili Mungu awape Hekima na Ufahamu katika kazi yao na kusimamia haki

♦ Ombea kila Kiongozi Mkuu wa muhimili kadiri Roho Mtakatifu atakavyokuongoza.

2. Ombea viongozi wote watumie nafasi zao kutoa haki ili amani itawale Tanzania tuishi maisha ya mshikamano na utulivu. Waefeso 6:12. Mithali 14:34. Warumi 13:1-7.

♦ Ombea Viongozi wa serikali kuanzia ngazi ya juu hadi chini.

♦ Ombea Ulinzi wa Mungu kwa kila kiongozi.

3. Ombea viongozi wote wa vyama vyote vya kisiasa. Watoe ushauri sahihi kwa serikali. Mithali 11:14

♦ Ombea Amani katika kazi zao za Kisiasa

♦ Tukatae roho za machafuko na uvunjifu wa amani.

4. Omba – Mungu atupe viongozi waadilifu. Danieli 2:21. Zaburi 33:10.

♦ Uadilifu kwa viongozi wote wanaoteuliwa na mamlaka husika.

♦ Uadilifu kwa kila mwenye dhamana ya uongozi.

Join the Discussion

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top